Get New DJ Mixes
AUDIO E NEWS

MSIBA MZITO DIDA AFARIKI DUNIA

Taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa aliyekuwa mtangazaji wa Wasafi Media, Khadija Shaibu maarufu kama Dida, amefariki dunia. Kwa mujibu wa taarifa hizo, kifo chake kimetokea usiku wa Oktoba 4, 2024, alipokuwa akipokea matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam.

Dida, ambaye alikuwa maarufu kwa kipindi cha Mashamsham kilichorushwa na Wasafi FM, alikuwa amelazwa hospitalini kwa matibabu kutokana na hali ya kiafya ambayo bado haijawekwa wazi kwa undani. Habari hizi zilitolewa kwa mara ya kwanza na mtangazaji mwenzake, Maulid Kitenge, kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa X (zamani Twitter). Kitenge alithibitisha kwamba Dida alikuwa akiugua kabla ya kufariki, lakini chanzo kamili cha kifo bado hakijawekwa wazi.